ESOSHI 2

BLOG HII IMEDHAMINIWA NA ESOSHI GENERAL TRADING COMPANY LTD WAKALA WA TANGA FRESH

TANGAZO

Sunday, May 19, 2013



Shirika hili la ndege katika safari za kitaifa na kimataifa


TOA MAONI/USHAURI EMAIL-rwasinaa@yahoo.com     Tuma sms  sim-                                      0782-164705  






 


   SEVERE MESIAKI THEONESTINA NA METHAL ZA KIHAYA







AJALI MBAYA YA  PIKIPIKI NA BAJAJI  JIJINI DAR JESHI LA WANANCHI LAPONGEZWA KWA UOKOAJI MEI 19/2013







Jeshi la wananchi Tanzania limepongezwa na wananchi kwa juhudi walioionyesha baada ya kutokea kwa ajali ya pikipiki na bajaji 19/05/2013 katika kituo cha  daladala cha kushusha na kupandisha abilia eneo la Makonde jijini Dar,ambapo wanajeshi  hao waliamua kuahilisha safari yao baada ya kuona tukio hilo na kuamua kuwaondoa majeruhi hao na kuwapakia kwenye gari lao kisha kuwapeleka hospitali ya Lugalo.Mtandao huu ulifuatilia kujua majeruhi hao wanapelekopelekwa na kushuhudia kuwa ni hospitali ya Lugalo,picha hizo hazikupatikana  ni kutokana na maadili yetu ya kikazi






Saturday, May 18, 2013

KAWAIDA  TUKIKAA MKAO HUU KUTUELEZE KUSUDIO NA SI VINGINEVYO

 

SIMBA NA YANGA  WAKIPAMBANA UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR MEI 18/2013

Katika d.k ya 05 mchezaji kiungo wa timu ya Yanga Kavumbagu ali ipatia goli la kwanza timu  yake  ambapo mpaka d.k 90 zinaisha timu hiyo iliibuka na goli mbili dhidi ya mpinzani wao  Simba  bila
 

 

POMBE AINA YA ULANZI ILIVYO "DILI" NJOMBE


 

 

 

 

NAIBU WAZIRI MAMBO YA NDANI, SILIMA AFUNGUA DUTY FREE SHOP YA KISASA YA JESHI MAGEREZA-MKOA WA DODOMA.Saturday, May 18, 2013 

 

Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini, Kamishna Jenerali John Minja akitoa hotuba fupi ya kumkaribisha mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima kufungua Supermarket (Duty Free Shop) ya pili ya kisasa ambayo imejengwa na jeshi hilo, katika Gereza Isanga, mjini Dodoma. Ufunguzi huo umefanyika leo mjini humo

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima akizungumza na maafisa magereza kabla ya kufungua Supermarket (Duty Free Shop) ya pili ya kisasa ya Jeshi la Magereza ambayo itawawezesha maafisa wa jeshi hilo, askari na familia zao kupata huduma ya kununua bidhaa mbalimbali kwa bei nafuu.  Kushoto ni Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini, John Minja na kulia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Military Shops ambaye ndiye aliyewekeza katika Supermarket hiyo, Afzal Meghji. 
 


Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Supermarket (Duty Free Shop) ya pili ya Jeshi la Magereza iliyojengwa katika Mkoa wa Dodoma




 Picha ya pamoja



Friday, May 17, 2013


AJIRA KWA VIJANA

 

FAINALI MISS UTALII TANZANIA 2013, KUFANYIKA JUMAPILI MKWAKWANI TANGA


Friday, May 17, 2013 


Washiriki wa Miss Utalii 2012/13 wakiwa katika picha ya 

Pamoja na 
Mkuu wa Wilaya pamoja na 
Viongozi wa chama na Serikali.
 

Luteni  Mstaafu Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mheshimiwa Chiku Galawa akiwasalimia Washiriki wa Miss Utalii 2012/13 wakati wa kuupokea Mwenge wa Uhuru Uwanja wa Mkwakwani


 Hatimaye fainali za Taifa za Miss Utalii Tanzania mwaka huu,zinafanyika mkoani Tanga siku ya Jumapili Tarehe 19-5-2013katika uwanja wa CCM Mkwakwani Tanga. Fainali hizo za tano za Taifa za mashindano ya Miss Utalii
  


Tanzania tangu kuanzishwa kwake mwaka 2005, zitajumuisha jumla ya warembo 30 kutoka mikoa yote ya Tanzania, na vyuo vikuu watapanda jukwaani kuwania taji la Taifa la Miss Utalii Tanzania 2012/13.

Zawadi kwa mshindi wa kwanza ni mkataba wenye thamani ya sh.90, 000,000/=,ambao unajumuisha skolashipu ya kusoma kozi ya Diploma katika chuo cha Dar es Salaam City Collage, safari za kushiriki mashindano ya Dunia,ziara za Tanzania Great Safari and Tour 2013, kugharamiwa usafiri wakati wa shughuli za kutekeleza majukumu yake ya ushindi,na shilingi 5,000,000/= baada ya kutumikia taji lake wakati wa kukabidhi kwa mshindi wa msimu ujao.

Aidha mshindi wa pili hadi wa tano, kila mmoja kila mmoja atajipatia mkataba wenye thamani ya shilingi 58,000,000/=, ambao pia unajumuisha skolaship za kusoma chuo cha Dar Es Salaam City Collage na safari za kushiriki mashindano ya kimataifa nay a dunia, pia ushiriki wa safari za Tanzania Greet Safari and Tour 2013 na kugharamiwa usafiri wakati wa utekelezaji wa majukumu yao ya ushindi. Washiriki walio bakia watajipatia tuzo mbalimbali za heshima, za utalii, utamaduni, jamii, uchumi, mitindo, ,wanyama pori,misitu,mazingira,utalii wa ndani,utalii wa kitamaduni,jinsia,utalii wa michezo,utalii wa mikutano,elimu ya jamii,afya ya jamii, urembo na maliasili.

Mashindano ya Dunia ambayo washindi hao watashiriki ni Miss Tourism World 2013, Miss Tourism United Nation 2013, Miss Tourism University World 2013, Miss Heritage World 2013, Miss United Nation 2013,Miss Freedom Of The World 2013,na Miss Globe International 2013.

Burudani katika fainali za mwaka huu ,zitakazo fanyika kitaifa mkoani tanga jumapili tarehe 19-5-2013, ni pamoja na Bendi ya Msondo Ngoma, Mwana mziki wa kimataifa Che Mundu Gwao, Ngoma za asili na vichekesho kutoka kundi la Majuto Arts Group linalo ongozwa na mwigizaji mahili na mkongwe Mzee Majuto,sarakasi na muziki wa kizazi kipya yani bongo fleva.Maandalizi yamekamilika, na hali ya kambi ni shwari huku washiriki wote wakiwa katika hali ya kujiamini, kila mmoja akijigamba kupeleka jaji mkoani kwake mwaka huu.

Katika shindano la mwaka huu, katika ukumbi wa CCM Mkwakwani, wabunge ,madiwani,wakuu wa wilaya,na viongozi wa vyama na serikali wamealikwa kuhudhuria. Mkuu wa mkoa wa Tanga Mheshimiwa Chiku Galawa atakuwa mgeni rasmi katika fainaali hizo za kihistoria kufanyika mkoani Tanga.

Tumepeleka fainali za jumapili katika uwanja wa CCM Mkwakwani Tanga, ili kutoa fulsa kwa wakazi wa kada zote kushudia fainali hizo, kwani shindano hili ni kwa ajili ya watanzania wote bila kujali utofauti wao wa vipato wala umri,ndo mana viingilio ni vya beii ya chini sana, ambapo shindano litaanza  mchana wa saa 7 hadi usiku wa manane. Viingilio watoto itakuwa 2000/=, wakubwa mzunguko itakuwa shilingi 5,000/=, viti maalum shilingi 20,000/= na viti vya kawaida ni shilingi 10,000/=.

Shindandano la mwaka huu limedhaminiwa na TANAPA,DAR ES SALAAM CITY COLLAGE, ORIENTAL BUREAU DE CHANGE, MTWANA CATERING, MAGAPIE DISTRIBUTORS,SOPHIA PRODUCTION,NCAA, CCM MKOA WA TANGA,MBASHA ENTERTAINMENT,IKONDELELO LODGE,PANGU ENTERPRISES,BODI YA UTALII TANZANIA (TTB),BARAZA LA SANAA LA TAIFA (BASATA), CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM - SHULE KUU YA UANDISHI WA HABARI TANZANIA (TSJMC).

Miss Utalii Tanzania ni Alama ya Urithi wa Taifa – Utalii ni Maisha Utamaduni ni Uhai
Asante,
Erasto Gideon Chipungahelo
Rais

 



SHUKRANI

 MAREHEMU BWANA WILLIAM VEDASTUS MUGURUSI

(1943 – 2013)

Familia ya Marehemu, Bwana William Vedastus Mugurusi wa Kijitonyama Dar es Salaam, inapenda kutoa shukurani zake za dhati kwa wale wote walioshiriki nao katika kumuuguza na hatimaye kifo cha mume, baba, kaka na babu yao mpendwa kilichotokea siku ya Jumanne tarehe 16.04.2013 katika hospitali  ya AMI Wellness Center na kuzikwa Ijumaa tarehe 19.04.2013 katika makaburi ya Kinondoni Dar es Salaam.
Shukurani za pekee ziwaendee madaktari wote na wauguzi wa hospitali za Apollo,(India) Aga Khan na Ami Wellness Center ambao walijaribu kwa kadri ya uwezo wao kuokoa maisha ya mpendwa wetu; Uongozi na timu nzima ya Globe Accountancy Service (GAS) kwa ushirikianao wao wa hali na mali; Mapadri na wahudumu wote wa Kanisa Katoliki kwa huduma za kiroho; AAR, FHI360, ndugu, jamaa, marafiki, wanajumuiya ya Mt. Damiano Mfia Dini, na majirani wote.
Kutokana na ukweli kwamba siyo rahisi kumshukuru kila mmoja kwa jina, tunapenda kuwahakikishia kwamba tunathamini ushiriki wa kila mmoja kwa njia ya pekee, ushiriki ambao umeendelea  kutupa faraja wakati wa kipindi hiki kigumu. Tunawasihi tafadhali kila mmoja apokee shukrani zetu za dhati katika uzito ule ule.
Kutakuwa na misa ya shukrani tarehe 25 May 2013, saa 4 asubuhi nyumbani kwa marehemu William Vedastus Mugurusi, Kijitonyama.  WOTE MNAKARIBISHWA.


RAIS KIKWETE ALIPOZINDUA KAMPENI YA LISHE

Thursday, May 16, 2013 
 
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizindua   kitabu cha kampeni ya Lishe Tanzania baada ya kukizindua leo Machi 16, 2013 katika bustani ya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam. Kulia ni Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe Peniel Lyimo akifuatiwa na Mkurugenzi wa kwanza wa Taasisi ya Chakula na Lishe Mzee Lema. Kushoto ni Mama Salma Kikwete akifuatiwa na Mama Maria Nyerere
 
 Mama Maria Nyerere akifurahia tuzo maalumu aliyopokea kwa niaba ya Baba wa Taifa aliyotunukiwa na Taasisi ya Chakula na Lishe kwa mchango wake mkubwa kwa kukuza na kuendeleza sera ya lishe nchini wakati wa sherehe za uzinduzi wa Kampeni ya Lishe Tanzania leo Machi 16, 2013 katika bustani ya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam.

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Naibu Waziri wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Seif Rashid akisalimiana  kitabu cha kampeni ya Lishe Tanzania baada ya kukizindua leo Machi 16, 2013  katika bustani ya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam. Kulia ni Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi na kushoto ni Mama Salma Kikwete akifuatiwa na Mama Maria Nyerere


 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi tuzo maalum iliyotolewa na Taasisi ya Chakula na Lishe kutambua mchango wake mkubwa katika kusimamia lishe na maendeleo yake  nchini  katika uzinduzi wa kampeni ya lishe nchini  leo Machi 16, 2013  katika bustani ya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam. Kulia ni Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi na kushoto ni Mama Salma Kikwete akifuatiwa na Mama Maria Nyerere


 

Wednesday, May 15, 2013

BUNGENI


Waziri wa Viwanda na Biashara,Dr. Abdallah Kigoda akiwasilisha bajeti ya Wizara yake Bungeni Mjini Dodonoma May 15,2013.
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta na Mbunge wa Arusha Mjini , Godbless Lema, Bungeni Mjini Dodoma May 15,2013. (picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Meneja Mkuu wa Kampuni ya AVIC International Ya Beijing China, Bibi Yab Qiong (watatu kushoto), Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Masoko wa Kampuni ya CATC ya Beijing China, Johnson Wang (wapili kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya CATIC nchni, Bw. Simon Xu, ofisini kwake mjini Dodoma, May 15, 2013. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Msondo,Che Mundugwao,Majuto kuwasha moto Fainali za Taifa Miss Utalii Tanzania Mkwakwani Tanga tarehe 19.05.2013.

Warembo wa Miss Utalii Tanzania 2013 wakiwa katika Picha ya Pamoja

Baada ya shamlashamla na mapokezi makubwa ya Miss Utalii Tanzania walipo ingia Mkoani Tanga na kupokelewa na umati mkubwa wa watu, warembo hao wapo kambini tayari kwa maandalizi ya Fainali hizo.

Fainali za Taifa Miss Utalii Tanzania zitafanyika Tarehe 19.05.2013 Mkoani Tanga ambapo warembo zaidi ya 30 watapanda Jukwaani kuwania Taji la Taifa la Miss Utalii Tanzania 2013 ndani ya Mkwakwani.

Sambamba na Fainali hizo za Miss Utalii , kutakuwa na Burudani ya Kukata na shoka ambayo itasindikizwa na Bendi kongwe ya Muziki Msondo Ngoma kutoka Dar es salaam, Mwanamuziki wa Kimataifa Che Mundugwao, Majuto Arts Group, Mdumange, vikundi vya ngoma na Sarakasi.

Fainali za Taifa zitaanza kuanzia saa 7 mchana hadi saa 12 jioni Ambapo viingilio kwa watoto itakuwa 2,000 na wakubwa 5,000 Baada ya hapo kuanzia saa 1 usiku hadi Majogoo viti Maalum itakuwa ni 20,000 na kawaida itakuwa 10,000 

Mpaka sasa Kambi ya Miss Utalii Tanzania 2013 ipo jijini Tanga Mwambani Hotel na inaendelea Vizuri, Warembo zaidi ya 30 kutoka mikoa yote nchini ,wanajiandaa vizuri  kwa ajili ya Fainali Hizo zitakazo fanyika wiki ijayo Tanga, Kanda Maalum ya Zanzibar na Vyuo vikuu Tanzania.


Washindi wa 1-5 wa Fainali za Taifa ,watawakilisha Tanzania katika mashindano mbalimbali ya Dunia na nchi yatakako fanyika katika mabano  International Miss Tourism World (Marekani), Miss Tourism United Nation (Mexico), Miss Heritage World (Tunasubiri Taarifa), Miss Tourism University World(Tanzania), Miss Globe International (Uturuki), Miss Tourism World ( Equatorial Guinea ), Miss Freedom Of The World ( Kosovo) , na Miss Tourism United Nation (Nigeria)  n.k

Wakati huohuo, katika kuhakikisha kuwa maandalizi ya Fainali za taifa, za mashindano hayo ambapo mkoa wa Tanga unakuwa wenyeji kwa mara ya kwanza yanafanyika kwa ubora na hayakwami, kamati ya maandalizi ya kimkoa umeundwa ambayo mwenyekiti wake ni Peter Semfuko Afisa Utamaduni wa Jiji la Tanga. Miss Utalii Tanzania ,hadi sasa tunashikilia Jumla ya mataji 5 ya Dunia na kimataifa, yakiwemo ya Miss Tourism World 2005-Africa,Miss Tourism World 2006-SADC,Miss Tourism World 2007-Africa, Miss Tourism
Model Of The World 2008-Personality, Miss Africa 2006 – 1ST Runner Up n.k